Wikipedia Ya Kiswahili
BLOGU YA KISWAHILI KWA AJILI YA KUSAFISHA FIKRA ZA WAAFRIKA!
Niliandika muhtasari huu hivi majuzi kwa ajili ya blogu ya Sauti za Dunia (Global Voices) kuhusu mkutano niliohudhuria majuzi kule Helsinki, Ufini. Usome kwa kubonyeza hapa.
Nadhani hadi "mwokozi" akija mara ya pili atatukuta wanadamu tuko kwenye mikutano. Wanadamu tunapenda sasa kukutana...na kuongea na kupanga mikakati. Bila kusahau kula na kunywa mvinyo.
Mambo mengi yametokea na yanaendelea kutokea toka niandike mara ya mwisho. Yapo ambayo nisingependa yakupite. Kwanza kabisa leo hii kutakuwa mahojiano kati ya mkurugenzi wa masuala ya mtandao wa Wanahabari Wasio na Mipaka, Julien Pain, kuhusu kitabu kizuri sana walichokitoa kuhusu uanaharakati wa mtandaoni. Kitabu hiki ambacho ni kiongozi cha wanablogu na wanaharakati wa mtandaoni kinapatikana bure hapa. Mtu yeyote anaweza kushiriki kwenye mahojiano hayo ambayo yatafanyika kwa kutumia teknolojia ya Internet Relay Chat (IRC). Taarifa kamili kuhusu saa na jinsi ya kuingia kwenye mtandao huo wa IRC nenda hapa.
Kati ya mijadala iliyokuwa mikali ni ule kuhusu rushwana maendeleo. Ilikubalika kuwa moja ya chanzo kikubwa cha rushwa katika jamii mbalimbali duniani ni rushwa. Ami Mpungwe wa Namitech East Africa alidai kuwa tofauti na mtazamo wa wengi rushwa sio tatizo la nchi masikini tu. "Tatizo ni kuwa rushwa ikitokea nchi tajiri inaitwa kashfa, ikitokea nchi masikini inaitwa rushwa," alisema.
Haya, ndio mkutano umefungwa hivyo. mabango yanaondolewa. Viti vinakusanywa. Vitambaba vya mezani vinakujwa. Picha zinapigwa. Anuani kubadilishana. Mvinyo wa mwisho mwisho. Na karanga pia (ila mpishi kazimwagia chumvi kabisa).


** Picha na Muhidin Issa Michuzi.

Marais Benjamin Mkapa wa Tanzania na Tarja Halonen wa Ufini wakiongea asubuhi hii. Marais hawa wamesisitiza kuwa muundo wa kisiasa na kiuchumi duniani unahitaji kubadilishwa. Mkutano wa Helsinki ni hatua muhimu katika kutafuta namna ya kujenga duniani ambayo inajali utu na haki za msingi za binadamu. Umuhimu wake unatokana na ushirikishwaji wa washikadau wa sekta mbalimbali.
Siku ya Blogu Duniani nilichagua, kama jinsi taratibu za siku hiyo zilivyokuwa, wanablogu watano. Baadhi yao wamesema haya:


Jumatatu ijayo ninaondoka kwenda kwa Wafini (nchini Finland). Nitakuwa katika jiji la Helsinki kushiriki na kublogu mkutano wa Helsinki 2005 kupitia mradi wa Sauti ya Dunia na Wizara ya Mambo ya Nje ya huko Ufini.. Kwa kuwa mkutano huo unahudhuriwa na rais anayemaliza muda wake na pia rais ajaye wa Tanzania, huenda nikapata nafasi ya kunywa nao kahawa kujadili "maendeleo" ya nchi.
Nilikuwa natazama wanablogu wa Kiswahili walioshiriki kwenye siku ya blogu duniani. Katika pitapita nimekuta kumbe kuna mwanablogu wa Kiswahili aliyechaguliwa. Mawazo na Mawaidha katika orodha ya wanablogu wake watano amemchagua mwanablogu mpya wa Kiswahili. Huyo ni mtaalamu wa uchawi wa kizungu, ndugu Swai. Blogu ya Swai sijui jinsi ya kuielezea. Ninadhani Swai ni mpenda ucheshi sana.