12/03/2005

Nafasi ya Kazi Katika Mradi wa Sauti za Dunia

Kutokana na kupanuka kwa shughuli za mradi wa Sauti za Dunia, mradi huo umetangaza nafasi ya kazi ya mhariri mtendaji. Atakayeajiriwa kwa kazi hii hatahitajika kuhama anakoishi hivi sasa. Hii ni kazi utakayoifanya kupitia mtandao wa kompyuta. Bonyeza hapa usome wanatafuta mtu wa namna gani (kama unafahamu mtu atakayefaa unaweza kumtumia habari hii kwa kubonyeza kwenye picha ya bahasha pembeni mwa sehemu ya kutolea maoni).

2 Maoni Yako:

At 12/05/2005 08:38:00 AM, Blogger Jeff Msangi said...

Ndesanjo,
Nimeliona tangazo,ningefurahi kuona mwanablogu mwenzetu yeyote yule anaomba kazi hii.Jambo moja tu sijaliona,hii kazi ina malipo yoyote au ni ya kujitolea?

 
At 12/05/2005 08:40:00 AM, Blogger Jeff Msangi said...

Samahani nimeona jibu nililolitaka.Kuna malipo kutokana na uzoefu.Wakati mwingine akili zangu naona zinakimbia badala ya kutembea.

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com