11/30/2005

Vyombo vya Habari au Vyombo vya Uongo?

NYONGEZA!!!!!: Nilipoandika habari hiyo hapo chini mapema leo sikuelezea jambo fulani muhimu sana. Ni kwamba serikali ya Marekani imetoa hela kwa kampuni ya Lincoln Group. Kampuni hii inachukua "habari" zilizoandikwa na wanajeshi wa Marekani kisha inazitafsiri kwa Kiarabu kisha inalipa magazeti ya Iraki ili iyachapishe kwa majina tofauti na yale ya askari wa Marekani walioandika. Na huu ndio uhuru, na hii ndio demokrasia ambayo Marekani inataka kusambaza duniani!
*******************************
Nina tabia ya kuviita vyombo vya habari, "vyombo vya uongo." Usidhani kuwa sina sababu za msingi. Sasa huu ni mfano mmoja. Kampuni iitwayo Lincoln Group imekuwa ikilipa wafanyakazi wake ili wajifanye kuwa ni waandishi wa habari na kuandika habari katika magazeti ya nchini Iraki. Habari hizo nia yake ni kuhadaa akili za Wairaki ili waamini kuwa Marekani ni mkombozi wao na sio mwizi wa mali yao ya asili. Yaani wanachofanya hawa jamaa ambao wanalipwa na serikali ya Marekani ni kupandikiza uzushi kwenye magazeti. Bonyeza hapa usome habari yenyewe.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com