11/21/2005

Kura ya Maoni Kenya: Wana Machungwa Wanaongoza

Wapiga kura wa upande wa machunga ambao unakataa katiba mpya inayomlimbikizia Rais madaraka wanaongoza. Wanaounga mkono katiba hiyo (wanaotumia alama ya ndizi) wanaongozwa na Rais Kibaki ambaye wakati akiwa nje ya madaraka alitaka Kenya iwe na katiba ambayo haitampa mtu mmoja madaraka makubwa. Lakini alipoingia madarakani...au kwenye utamu kama mnavyojua...anataka alimbikiziwe madaraka kama vile yeye ni Mungu. Wanaosema "Hapana" wanaongoza kwa asilimia 56.

1 Maoni Yako:

At 11/22/2005 08:20:00 PM, Anonymous Anonymous said...

habari za kenya za nini? Tanzania yetu tuu inatushinda.

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com