12/07/2004

MWANAHARAKATI WA MTANDO WA TARAKILISHI AACHIWA

China ni kati ya nchi ambazo zinaogopa sana mapinduzi ya zana mpya za habari na mawasiliano. Zana hizi, wavuti (internet), barua pepe, blogu, simu za mkono, n.k., zinawezesha wanaharakati kuwasiliana, kupeana habari, kuripoti udhalimu na mambo mengine mengi kwa haraka na gharama ndogo. Mwanaharakati wa mtandao wa tarakilishi aliyekuwa amefungwa na serikali inayojiita ya Kikomunisti ya China amefunguliwa. Nenda hapa. Hata hivyo huyu bwana hataruhusiwa kurudi kwenye kazi yake ya ualimu na wala hana ruhusa ya kuandika kwa miaka miwili. Sasa sijui itabidi akale polisi, au atajaza mwenyewe...

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com