11/06/2005

Mwanablogu Mpinga Uislamu Atiwa Ndani

Abdolkarima Seliman ni mwanablogu toka Misri anayefahamika kwa kupinga vikali udhalimu wa serikali ya Misri na pia mapungufu katika dini ya Uislamu. Blogu yake imemtia matatani. Hivi sasa yuko jela na wanaharakati duniani hivi sasa wanaendesha kampeni ya kutaka aachiwe. Baadhi ya wanakampeni hao wanasema kuwa hawakubaliani na mawazo ya Abdolkarim ila wanaamini kuwa ana haki ya kujieleza. Tazama habari yake toka Kamati ya Kulinda Wanablogu kwa kubonyeza hapa. Pia habari yake iko katika blogu ya mradi wa Sauti za Dunia. Bonyeza hapa na hapa. Ukitaka kusoma blogu ya Abdolkarim bonyeza hapa. Ila lazima uwe unafahamu Kiarabu (na kwa taarifa yako Kiarabu sio "Kiislamu" kama baadhi ya watu wasemavyo. Kiarabu ni lugha na Uislamu ni dini ya Waarabu.)

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com