10/20/2005

Pop!Tech: Carolyn Porco

Aliyeko jukwaani sasa ni Carolyn Porco, mtafiti wa masuala ya sayari na anga za mbali. Anatuonyesha picha ya chombo kinachokwenda kufanya utafiti angani chenye ukubwa sawa na basi la kutoka Mwenge kwenda Kariakoo. Saa ni picha ya sayari ya Zohari na ule mkanda ulioizunguka.

Nimepitwa na mambo anayoongelea Carolyn, nimehama nikaingia kwenye ukurasa wa kamusi elezo ya Kiswahili kutafuta kama tuna majina ya sayari, nikajikuta nimeanza kuhariri kamusi hiyo. Sijui anachoongelea hivi sasa maana kaniacha mbali kweli. Lakini ngoja nisikilize kwa makini nijue kafika wapi.

Kwakuwa nimegusia kuhusu kamusi elezo ya Kiswahili. Niliomba tusaidiane kuijenga kamusi hii. Tutakuwa tunalalamika kila siku kuwa historia yetu inaandikwa na watu wengine wakati ambao tuna nafasi ya kuiandika wenyewe kwa kusaidia lakini hatutumii nafasi hiyo. Hivi sasa hakuna kamusi duniani zenye kutumiwa na watu wengi, mashuleni, vyuoni, watu binafsi kama kamusi huru (wikipedia). Utashangaa: watu wengi ambao wanaijenga kamusi elezo ya kiswahili hivi sasa ni wazungumzaji wa Kiswahili ambao wamejifunza ukubwani maana wametoka nchi za Magharibi.

Kamusi elezo ni ya ajabu sana. Unaweza ukajikuta umeandikwa au ukakuta jina la babu yako. Ni kamusi inaandikwa na watu na sio kundi dogo la wanazuoni wanaojifanya kuwa eti wanajua kila kitu. Unadhani kama sio hivyo pombe ya mbege ingekuwa kwenye kamusi elezo? Tazama hapa.

Narudi kwa mama Carolyn, kaniacha pale kwa Alfonsi, katikati ya majengo na kiboriloni wakati ndio anaitazama Chalinze...

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com