10/18/2005

Nakwenda Mkutano wa Pop!Tech kule Camden

Kila mwaka, shirika lisilo la kiserikali, Pop!Tech, huandaa mkutano mkubwa unaojumuisha wafanyabiashara, waandishi wa habari, wanazuoni, wataalamu wa teknolojia mbalimbali, wanaharakati, watunga sera, n.k. Mkutano wa kwanza ulikuwa ni mwaka 1997. Katika mkutano wake wa mwaka huu huko Camden, Maine, Pop!Tech kwa kushirikiana na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Masuala ya Michezo kwa ajili ya Amani na Maendeleo na kampuni ya teknolojia ya Sun Microsystems wamechagua Waafrika 12 (Pop!Tech/Sun Africa Fellows) ambao kwa njia moja au nyingine wanajihusisha na juhudi za kunyanyua bara la Afrika katika nyanja za teknolojia na jamii.
Katika Waafrika hao 12 kuna Watanzania wawili. Mmoja wa Watanzania hao waliochaguliwa ni Neema Mgana. Neema ni mwanaharakati wa masuala ya Ukimwi nchini Tanzania. Yeye ni mmoja wa wanaharakati wanawake 1000 waliochaguliwa kwa ajili ya Nishani ya Nobeli ya Amani. Soma habari hiyo hapa. Na kuhusu Nishani ya Nobeli kwa wanawake 1000 soma hapa.
Mtanzania mwingine aliyechaguliwa ni jamaa moja mwenye "rasta" anaitwa Ndesanjo Macha.
Kati ya waliochaguliwa pia yumo yule mwanablogu wa mstari wa mbele wa Kenya, Kenyan Pundit.
Orodha kamili ya Waafrika hao bonyeza hapa.
Na kuhusu mkutano huo bonyeza hapa. Tazama orodha ya watakaozungumza na masuala watakayozungumzia. Orodha hii ina watu ambao nawafuatilia sana kazi zao. Bonyeza hapa uwaone.
Kwa mtaji huo kesho jioni ninaondoka kwenda Camden, mji wa kihistoria ambako ndipo mkutano huo utafanyika. Na ninataandika juu ya mkutano huo hapa nikiwa huko.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com