10/18/2005

Maoni ya Watanzania Wanaokunwa na Uozo: Mkapa Kafanya Makubwa?

Kayonko Jumaa kaandika nasaha zake kuhusu nchi yetu ambayo naambiwa kuwa iliposwa na kuolewa siku nyingi sana. Nasaha za Kayonko kazitoa kwenye ukurasa wa majadiliano wa Watanzania walioko Japan (TIJA). Naweka ujumbe wake wote na baadaye nitaweka nasaha za washiriki wengine katika mjadala huu kuhusu nchi yetu (yetu?). Ndugu Kayonko mimi simfahamu na waraka huu hajanipa yeye. Na ruhusu sijamuomba. Nimepewa na mzalendo mwingine ambaye anaamini kuwa Kayonko hatatia unaa kwa kuweka waraka wake kwa Watanzania hapa. Haya msome:
Watanzania wenzangu mmeutonesha Moyo wangu juu yaTanzania! Kuna siku huwa nasema Mungu ambaye kwa hakika nakilikusema alitupendelea na Tanzania yetu, yawezekana akatuingiza motoni watanzania wote kwa kushindwa ku-appreciate utajiri wa kila kitu alicho tupa. Naomba mnivumilie, nahisi hii barua pepe yangu itakuwa ndefu kwa sababu nadhani naongea kwa watu wenye uchungu na TZ yetu, walio free na siasa za kimangimeza, mchumia tumbo au ambao wanadhani FutureYetu ipo WEST.
Mimi huwa si waelewi watu ambao huwa wanasema eti Mkapa kafanya mambo makubwa kwa TZ, karudisha heshima yaTaifa kimataifa n.k. Hao ni wale ambao hawajui walisemalo daima milele lakini kama watapewa TuitionClass wakaelewa, wasubiri muda si mrefu udhaifu wa uongozi wa awamu ya tatu na sisiemu kwa ujumla utaonekana muda simrefu. Unajua mtu mwenye njaa yamuda mrefu ambaye hata ratiba yake ya kura haieleweki(yaani yeye kifungua kinywa cha viazi ndo lunch, na dinner ndo breakfast na siku zingine ni deshi) ukimpa msaada kidogo, si ajabu akakufuru kwa kukuita weweMungu. Mmeandika mengi sana kuhusu vibweka vya uongozi wetu, sasa mimi nitapita humo humo ni paraphrase na kusherehesha. Mwaka jana katika ukumbi wa AICC kule Arusha, nikiwa pamoja na wenzangu wa UDASM, Makerere na Nairobi varsity kwenye mafundisho ya "Future EastAfrican Leaders", hii ni Summer School ambayo hutolewana East African Uongozi Institute. Si kuamini macho na masikio yangu kwa majibu ambayo Kikwete (Huyu mgombeaUrais kupitia Sisiemu) nilipomuliza swali: Je, kamakweli nia ni kuondoa/kupunguza umasikini TZ mpaka mwaka 2025, hiyo 3% as royalty na 97% kwa wawekezaji itasaidia nini? (Na kwa taarifa yenu kama mjuavyo uzembe wetu (rushwa, ufisadi, kujuana n.k, hata hiyo3% ni namba tu si ajabu tunabaki na ziro point something %).
Kikwete alijibu kwamba: Ni mfumo tuliouchagua eti wa Market Economy na kama hatuwezi kuwavutia wawekezaji eti watajiondokea!!!!!. Kwa ufupi toka siku hiyo nilianza kuwa na wasiwasi juu ya uwezo wake kuliongoza taifa toka lindi la umasikini. Mpaka sasa wasiwasi huo bado ninao. Hajui hata hao wawekezaji ni watoto wa walewale wakoloni ambao walichota na kujenga nchi zao na kwamba kilichopo sasa ni muendelezo wa "BLOOD FED SYSTEM:NEO-COLONIALISM/GLOBALISATION. Hakuna siku mzungu atakaa akupe bure wewe mbongo, ili iweje? Akikupa shilingi moja ujue atachukua sh. 3 hata baada ya miaka mitano. Sumaye wakati akitafuta kura ili agombee urais alisema moja ya malengo yake ni kulinda wawekezaji walioletwana awamu ya tatu wasiondoke nchini!!! Moja ya vitu ambavyo Wapambe wa Mkapa wanavyojivuniani miundo mbinu hasa barabara. Hiyo ni kweli imeboreka lakini lengo hasa ni kama lile la wakati wa ukoloni "All the roads and railways ran from the interior to the coast", nadhani mnajua reli ya kati haijajengwa kumsaidia Muha wa Kigoma bali kumbeba kama MANAMBA akazalishe kwenye mashamba ya mkonge, pia reli hiyo ilisafirisha mali (madini n.k) lukuki toka Congo.
Sasabarabara za Mkapa ni kwa ajili ya kuvutia WAWEKEZAJI nchini "Conducive Environment for Foreign Investors". Kwa hiyo mtanzania wa kawaida anafaidi by chance tu. Barabara nyingi zinaelekea kuliko na madini ili hao wawekezaji wavune pasina mwenyewe kwa gharama nafuu. Hoja nyingine ni eti Mkapa ameweza kukusanya kodi kwaufanisi sana kuliko miaka iliyipita!. Hapa pia ni kweli mapato ya kodi yameongezeka ila kwa mtu ambaye upo CRITICAL and CURIOUS hupaswi kulipongeza hilo kwa nguvu zote. Naomba mjue kwamba TZ na Afrika kwa ujumla tusingehitaji misaada toka nje kama kungekuwa na FAIRNESS katika International Systems. Hebu fikiria, tumeprivatise mashirika ya umma kwa bei za kutupa, tunatoa tax holidays za miaka mitano, wawekezaji wakofree sana kufanya watakalo e.g wanatuletea hadi mayai, matunda toka south africa. Kuku toka nje. Hivi mnajua kama kuna Wachina wanauza karanga katika mitaa ya soko la kariakoo? eti nao wawekezaji! Hoja yangu hapa ni kwamba ongezeko la mapato ya kodi linatokana na ujinga wetu au ukipofu wetu; hivi nani anaweza kushindwa kulipa kodi wakati faida ni ya kuzoa kutokana na kupewa mashirika na migodi bure? Yaani hii haihitaji kuandika research proposal ili ufanye utafiti. Kwa jinsi mambo yalivyo hapa TZ ni justifiable kusema "bila hata kufanya utafiti una haki ya kusema? angalau ktk maongezi ya kawaida. Hivi mnajua kwa nini Mkapa anawekwa kwenye majukwaa yakimataifa (e.g Kukaa katikati ya Bush na Blair kule Gleneagles, Scotland pia Uenyekiti wenza waUtandawazi?), nawauliza tena mnajua au na nyie ni kama watanzania wengi?. Kwa taarifa yenu kwa ufupi ni kwamba "THE MAN HAS VEHEMENTLY SOLD US". Na je mnajua kama BUSH baba ni sehemu ya BARRICK GOLD MINING CO.ambayo inamiliki mgodi wa Kahama? Halafu wanatupoza kwa viji misaada ambavyo kamwe havitotutoa ktk umasikini wetu bali ASPRIN tu za kutupoza maumivu.
Hivi Gadaff wa LIBYA ana nini zaidi ya mafuta ambayo na sisi tunayo? Jamaa yule amegeuza jangwa kuwa kijani, anazalisha mpaka anatoa food aids nje. Anatoa unemployment benefits kwa raia wake. Sisi tuna madini lukuki lakini hayana faida kwetu. Gasi ya songo songoilitoka moja kwa moja hadi Dar leo hii ndo wanafikilia kuwapa umeme wenyeji wanaozunguka mradi. Ni ajabu na kweli, na inahuzunisha. Kama haya madini na rasili mali tulizonazo hayawezi kututoa ktk umasikini huu, faida yake ikatuwezesha ku-import "Appropriate Technology", yakatufanya tujenge strong infrastructures both social and physical, tukaweza kujenga mfumo imara wa elimu, pia tukajenga strong industrial base, basi kamwe maendeleo angalau ya kama nchi za Asian Tigers itakuwa ni ndoto na badala yake itakuwa ni vita baina yetu kama ilivyokuwa Angola, Ivory Coast, DRC n.k. Hii siyo kitu cha kuombea ila it is a material fact of which both the contemporary and ancient historical observationsin many parts of the world reveals. Si kwamba watu wanapenda vita ila kuna wakati hiyo inakuwa ndo the only way to reach their desired Destination and future. Ongea au fuatilia historia ya Rais mpya waBurundi, Peter Nkurunziza. Burundi na hata Rwanda si kwamba ni ukabila tu, uchumi wa kibaguzi daima hauvumiliki. Mimi nimesoma historia, hata hizo nchi za zilizoendelea zinajua lakini, la msingi kwao ni kupora tu. Wala amani tuliyonayo si kitu cha kujivunia sana kwani wao muhimu sana, angalia DRC na zamani Angola uporaji ulikuwa wa juu sana hata watu wakiwa wanauana tena kwa silaha toka Majuu! Kwetu sisi hapa TZ amani inakuwa muhimu zaidi kwa ajili ya DIRECT FOREIGN INVESTMENTS(DFI) otherwise mzungu hajashindwa kuchukua anachokitaka popote Africa iwepo amani au vita yeye hajari, kwa sababu yeye anacho kifanya ni ku-sustain vita huku akipora. USA ana uzoefu wa kufaidika na vita nje ya ardhi yake. Vita zote kuu mbili za dunia zilimpa uchumi imara na kuchukua nafasi ya UK, the former "Workshop of the World". Hata hizi DFI hazina faida sana kwa uchumi wetu. Mojatumeamini kwamba duniani kuna kitu kinaitwa FREE TRADEor OPEN ECONOMY na hivyo tumeshindwa kuwalindawazalishaji wa ndani, hatuna STRONG PROTECTIONISM POLICY ambayo kila taifa lililoendelea duniani lazima liwe nayo. Mmesikia juzijuzi jinsi ambavyo Marekani alikuwa anahaha kuhakikisha China anapunguza supply ya bidhaa za nguo huko Asia! Ili DFI ziwe na faida kwa local economy lazima zi-stimulate domestic economy na kutoa ajira zaidi angalau kwa kujenga viwanda vya vipuri nchini. Siyo kila spare-part lazima itoke ulaya. Nimeandika sana ingawa siwezi maliza yote kwani upuuzi ni mwingi sana Afrika hasa TZ linapokuja suala la maendeleo. Hebu tuone aibu jamani nchi kama Ivory Coast pamoja nakuwa na vita tayari watakuwa Ujerumani kwenye WORLD CUP sisi na amani yetu tu? Kwa nini haitusaidii kufanya lolote la kimaendeleo?
Wachache matajiri wengi masikini, amani amani; hii ni amani feki. Niongee kidogo kuhusu uchaguzi maana upo karibu. Kuna kila dalili kwamba kama uchaguzi utakuwa huru na waHaki, basi wabunge na madiwani wa upinzani wataongezeka, na hiyo itakuwa ni hatua muhimu ktk kuelekea kupata viongozi wanaojali na pia utawala bora. Kwani hao ndo tunawakosa hapa TZ. Binafsi sijali kiongozi ni wa CCM au Upinzani la msingi kwangu ni Maslahi ya Taifa. Mungu ibariki Tanzania, pia utusaidie tuwe na amani yakweli kwani hii tuliyonayo ni ya nta.
Kayonko Juma.

2 Maoni Yako:

At 10/18/2005 06:44:00 AM, Blogger Indya Nkya said...

Kama unataka kipimo kizuri cha kujua jinsi wananch wanavyoumia na mfumo wa soko, basi usikae ukiumiza kichwa chako kwenda kufanya utafiti, njia rahisi sana ni kuangalia jinsi rais wa nchi anavyosifiwa na nchi za magharibi. Anavyokaribishwa na kupigwapigwa mgongoni na Kichaka. Ukiona hivyo ujue mwananchi kaisha. wasikudanganye kwamba kuna njia nyingine ya kupima. hata akiwa profesa ambaye naye kashaoshwa ubongo wote kwa kutumia "indicators" za magharibi, Mkatalie. Mwambie kipimo ni hicho tuu. Suala la kodi nalo linachekesha mno. Hakuna hata mwaka mmoja mmoja ambapo tarakimu za pato la taifa kwa ujumla hazionekani kuongezeka (Nominal GDP)Kwa hivyo tunavyoambiwa makusanyo yameongezeka toka Bilioni 25 mwaka 1995 na kufikia sijuhi bilioni 120 kwa mwezi sasa hivi, sioni ajabu yoyote. Nominal GDP mwaka 1995 ilikuwa ngapi na sasa ni ngapi? Kodi kama asilimia ya GDP sasa hivi inakaribia asilimia 13 mwaka, 1995 sikumbuki ilikuwa ngapi. Lakini haipishani sana. Tuangalie sasa. Hizo bilioni 25 kwa mwezi ziliweza kununua bidhaa na kulipia huduma kiasi gani na sasa hizo bilioni 120 zinalipia kiasi gani? Tukishafika hapo tutajua kuna kiasi gani kimeongezeka.

 
At 10/19/2005 12:56:00 AM, Blogger Egidio Ndabagoye said...

Mimi nasikitika sana kuona kuwa kuna Watnzania wengi sana ambao hawajuia kipimo cha Raisi wao kafanya nini kwa kipindi miaka aliyokaa madarakani. Cha kushangaza zidi hata wasomi wachache ambao wananchi wanwategemea kutoa takwimu za uhakika nao pia wamelala usingizi Kuna.Wasomi wengi sana Wa Kitanzania hawajui kupima uchumi umekuwa vipi?.Raisi Mkapa kila kukicha hadidhi zake ni kuhusu barabara mara daraja ni vile vitu vidogo ambavyo ni haki yake kuvifanya kama raisi.Kwenda kukaa meza moja na wakina Kichaka ndio kipimo cha Watanzania kujulikna kimtaifa? atuambie kule Uskochi ametuletea ahueni gani sisi Watanzania.Kuwa mwenyekitim mwenza sijui wa Utandawazi sisi tunafaidika nini nae.Amewandaa vipi Watanzania na UTANDAWAZI.Nikiasi cha mtu kutokuwa na Shahada ili kuweza kutambua haya maigizo ya Mkapa na Serikali yake.Hizo barabara mbona hazipo sehemu kusikokua na uwekezaji kule kwa wapoiga kura wake hakuna kitu wanchokiita "barabara kiwango cha lami".Kuna sehemu nilikwenda tena sio mbali na "Tanzania" laki i lami hawajui ninini? wanaita chuma

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com