10/17/2005

Blogu nyingine ya Mtanzania hiyooooo....

Nakuapia vile...hakya nani vile...kila anapotokea mwanablogu mpya ninajisikia furaha isiyo kifani. Haya, kuna mwanablogu mpya Mtanzania. Huyu ni Fatma Karama. Ni mwanafunzi wa sheria pale kwa Bibi Lizabeta, Uingereza. Kwao Arusha. Ameanza kublogu kwa kiingereza, ingawa ataingilia pia na Kiswahili. Kama kawaida tunamtembelea na kumkaribisha. Bonyeza hapa umsome. Kuna somo ametoa ambalo nimelipenda sana (ingawa sikuelewa kwanini ametumia neno "superstition." Nadhani naweza kusema kuwa naelewa lakini pia sielewi...kama umenipata nasema nini). Somo hilo bonyeza hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com