11/07/2005

Jimbo la Rais Si Nchi Nzima?

Mtumishi wa sirikali kaniandikia waraka huu ambao unaonyesha matatizo yaliyoko katika mfumo wetu wa wizi wa kura (ambao tunauita mfumo wa uchaguzi). Barua yake hiyo hapo chini:

Mimi ni mtumishi wa Umma. Eneo langu la kazi ni kanda ya magharibi yenye mikoa ya Kigoma na Tabora. Tume ilitangaza kuwa kama italazimu watu wawe wamebadili vituo vyao mwisho mwezi Julai. Ghafla imezuka kazi inayonitaka kuja Kigoma kwa wiki kadhaa. Nimechukua kadi yangu ya kupiga kura. Kwa tafakuri tu ya kawaida nikajua sitaweza kuchagua wabunge au madiwani nikiwa Kigoma. Nikajua nitachagua Raisi kwa vile yeye jimbo lake la uchaguzi ni Tanzania nzima. Jana Tume ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza kuwa kama hutakuwa kituoni kwako huruhusiwi kupiga kura hata ya Raisi. Jambo hili limenishangaza na kunisikitisha sana. Iweje uwe ndani ya Taifa lako, ukiwa na haki zote za kupiga kura uzuiwe? La ajabu serikali yenyewe ndio imetutuma huku tuliko na sio kwa mapenzi yetu. Vipi Ndesanjo, wewe utapiga kura? Kama la mbona hujatoa kauli? (Gumzo?)

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com