8/31/2005

LEO NI SIKU YA BLOGU DUNIANI


Leo ndio ile Siku ya Blogu duniani. Wazo la kuwa na siku kama hii lilitoka kwa mwanablogu huyu hapa. Maelezo zaidi kuhusu siku hii yapo hapa kwa Kiswahili. Shukrani kwa Mawazo na Mawaidha aliyefanya tafsiri hiyo katika "wiki" maalum ya siku hiyo.

Siku hii wanablogu wanaopenda kushiriki wanachagua wanablogu watano ambao wanatoka katika tamaduni tofauti au wana mitazamo tofauti na yao.

Mimi nimechagua watu toka tamaduni tofauti. Sikupenda kutafuta watu kutokana na mitazamo yao. Wanablogu hao watano ndio hawa:

1. Mama wa Yousuf: Huyu ni mwandishi wa wa Kipalastina. Anaandika juu ya ulezi wa mwanaye na kazi ya uandishi katika nchi iliyokaliwa kwa nguvu na na Waisraeli. Kongoli hapa.

2. Jilltxt: Nimechagua blogu ya mwanataaluma, Jill, kutokana na blogu yake kuwa na viunganishi na habari nyingi kuhusu masuala ya uhusiano kati ya fasihi, taaluma, na blogu. Ninapenda watu wengi kufuatilia kwa undani juu ya mahusiano hayo. Ingawa toka apate kazi ya utawala, pamoja na kuendelea kufundisha, haandiki tena mara kwa mara, bado blogu yake ni benki ya taarifa nyingi na za kuelimisha. Kongoli hapa.

3. Blogu kuhusu uchaguzi wa wabunge Azerbaijan: blogu hii nimeichagua kutokana na ukweli kuwa wengi wa wasomaji wa blogu hii ni Watanzania na hivi sasa kampeni za uchaguzi zimepamba moto Tanzania. Nimetaka kuonyesha jinsi ambavyo teknolojia hii inarahisisha kazi ya upashaji habari za uchaguzi. Kita hapa.

4. Bwana Afigani: Hii ni blogu ya jamaa aliyeko Afghanistani. Nimemchagua huyu kutokana na shauku ya kutaka kujua wanablogu katika nchi kama Afghanistani wanafanya nini. Uzuri mwanablogu huyu anabandika picha hapa na pale, kwahiyo unaweza kuona hali ilivyo nchini humo. Kingita hapa.

5. Blogu ya kimbunga cha Katrina: Nimechagua blogu hii kwa nia ya kutaka kuonyesha jinsi ambavyo blogu zinaweza kutumika kutoa taarifa za haraka wakati wa maafa. Wakati wa maafa ya tsunami, blogu zilikuwa ndio chanzo kikuu cha habari na picha kwa haraka zaidi hata ya mashirika makubwa ya uongo (au habari kwa neno jingine) kama CNN. Nilikuwa natafiti wanablogu wanafanya nini kufuatia maafa yaliyoletwa na Katrina. Nenda hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com