8/26/2005

Blogu Nyingine za Watanzania Hizooooo...

Kwanza kabisa toka jumapili iliyopita nimekuwa nasikiliza wimbo wa Fela uitwao Trouble Sleep Yange Wake Am. Nimekuwa naupiga na kuurudia masaa yote. Ngoma za Tony Allen na mdomo wa bata wa Fela siwezi kuelezea. Katika wimbo huu kuna sehemu anasema:
Rafiki yangu katoka jela majuzi
Anatafuta kazi
Anazunguka huku na kule usiku na mchana
Polisi wamemsimamisha na kumwambia
Bwana nakukamata kwa kosa la kuzurura!
Hata sasa ninavyoandika ninasikiliza wimbo huu. Nimemtaja Fela kwa nia ya kuwaambia wasomaji walioniuliza maswali kadhaa juu ya Fela kuwa nitawajibu.
************************************************************************
Kuna wanablogu wapya ambao ukipata muda watembelee na kuwakaribisha. Kwanza kabisa yuko ndugu Swai. Swai anajitambulisha kwa namna ya pekee. Huu ndio utambulisho wake:

Nimetulia ni mtaalamu wa mambo flani ya uchawi wa kizungu si unaelewa iweje transistor itoe sauti au picha ya mtu...upo hapo babake...ndio mambo yangu hayo.

Ninaishi Mbezi beach ndani ya heka kumi nimejenga Jumba la kufa mtu naishi humo na mwanangu mmoja na Chui wangu pamoja na walinzi kumi na mbili ndani na nje. Nina gari ndogo za kutembelea kumi ambazo ni Range rover new model ya mwaka huu, Benzi S 500 jeusi lina seat za leather nyekundu,Jeep jeupe kali,Valnuet V2500 black,Ford Fury 3000, Free lander, Land crueser VX V12, BMW new model na nyingine nyingi sizikumbuki. Ninamiliki makampuni kibao hapa mjini yenye mitaji ya kuanzia billioni 100 na kuendeleaYaani kwa kifupi nina pesa ya hatari. Nina utaratibu wa kutoa misaada kwa waitaji jaribu kuniona nikusaidie lakini msaada usizidi bilioni 50.
Huyo ndio Swai.
Mwanablogu mwingine anayeandika kwa kiingereza ni ndugu Peter John. Mtembelee hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com