8/26/2005

Siku ya Blogu Duniani: Tarehe 30 Mwezi Huu

Mwanablogu toka Israeli, Nir Ofir, ndiye aliyetoa wazo la tarehe 31 mwezi wa nane kuwa ni siku ya blogu duniani. Wazo hili lilimjia pale alipotambua kuwa tarehe 31 Agosti ikiandikwa hivi "3108" inaweza kusomeka kama neno "blog." Halafu anasema kuwa amegundua kuwa ingawa mtandao wa kompyuta umeelezewa kuwa utasaidia kuifanya dunia kuwa kijiji, hali halisi inaonyesha kuwa (akitumia mfano wa wanablogu) kuwa wanablogu wanasoma wanablogu wale wenye mawazo kama yao au waliotoka katika nchi zao. Hata viunganishi tunavyoweka kwenye blogu ni vile vya wanablogu wenye mawazo au mitazamo kama yetu.

Basi akaona kuna haja ya kuwa na Siku ya Blogu Duniani. Na ndio hiyo tarehe 31 mwezi ujao. Katika siku hiyo unachotakiwa kufanya ni kuwatambulisha wanablogu watano ambao wametoka katika utamaduni tofauti na wako na pia wana mitazamo tofauti na yako.

Mradi wa Sauti ya Dunia unazungumzia pia siku hiyo.

Nawasihi wale wanaoweza washiriki.


0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com