11/03/2004

NIACHENI KWANZA NIPUMUE

Naombeni mnipe muda wa kupumua, kula, kulala, na kutafakari. Kwanza nataka kuhakikisha kuwa niko macho. Sijalala na wala sioti. Nasikia kuwa Joji Kichaka kawa tena rais wa Marikani. Kashinda kura za umma na kura za chuo cha kura. Ataongoza kwa miaka mingine minne. Hapana, nipe muda kidogo. Sina la kusema zaidi kwa sasa. Kuna wanaohamia Canada. Kuna wanaolia. Kuna wanaocheka. Nifunge virago kurudi kijijini Moshi? Kuishi miaka minne ndani ya serikali na bunge la kihafidhina sio mchezo jamani. Hapana, nipe muda. Ngoja nikasafishe uso isije ikawa ninaota au labda luninga yangu inanichezea shere!

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com