10/31/2004

UNGO NA UNUNUZI WA NDEGE YA RAIS

Kuna mjadala mtamu sana unaendelea juu ya ununuzi wa ndege ya Rais wa Tanzania. Nadhani ili watu wengi wafaidike na mjadala wenyewe, nitaweka maoni ya watu mbalimbali waliochangia na wanaoendelea kuchangia ndani ya blogu hii. Mjadala ni moja ya nguzo za demokrasia: Kujadili, kushawishiana, kukubaliana, kukataa kukubaliana, n.k.
Sijachangia lolote katika mjadala huu. Nina swali dogo ambalo ninatafuta jibu lake kabla sijaingia rasmi mjadalani. Hivi kwanini wachawi wa Tanzania wasisaidie taifa letu kwa kumpatia Rais ungo wa kusafiria?

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com