10/31/2004

BUSH NA KIINGEREZA

Rais mwizi wa kura, Joji Kichaka, anaandamwa na wapinzani wake kwa tuhuma kuwa hana kitu kichwani. Wanadai huyu jamaa shuleni mambo yalikuwa hayapandi hata kidogo. Moja ya vielelezo vya kuwa yeye ni mbumbumbu ni madai kuwa katika mjadala wa Urais alikuwa amevaa kidude cha mtandao usiwaya (wireless) ili awasiliane na mshauri wake Karl Rove, ambaye alikuwa akimnong'onezea majibu!
Wanadai pia kuwa ingawa Kiingereza ni lugha pekee anayoijua, lugha hii inampa tabu sana. Katika mjadala wake wa mwisho wa mwongo mwenzake wa chama cha Democratic, John Kerry, Bush alisema "internets" wakati ambapo neno internet halina wingi kwahiyo huna haja ya kuongeza "s" kama alivyofundishwa akiwa mtoto!
Ukitaka kuona picha ya kidude cha mtandao usiwaya alichovaa Joji Kichaka, kongoli hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com