10/29/2004

MTANZANIA MWINGINE KATIKA ULIMWENGU WA BLOGU

Pamoja na kubanwa na shughuli nyingi, zikiwemo za uchaguzi wa Urais wa hapa Marekani, nimeona ni vyema nichukue nafasi hii kutangaza kuwa kuna Mtanzania mwingine, Dennis Mponji, ambaye ameingia kwenye ulimwengu wa wana blogu. Blogu yake iitwayo FURAHIA MAISHA YAKO inaungana na blogu nyingine mpya ya Mtanzania Simon Mkina iitwayo KONA YANGU. Niliwahi kusema kuwa Wakenya kwa upande wa Afrika Mashariki ndio ambao wako mbele sana katika ku-blogu. Ninafurahi ninapoona Watanzania nao wanaanza kutumia teknolojia hii rahisi na nyepesi kujifunza kuwasiliana, kupeana taarifa, kutoa mawazo yao bila kuwa chini ya uangalizi wa mtu yeyote. Kongoli hapa kuiona blogu ya Furahia Maisha Yako. Bado iko kwenye ujenzi, siku zinavyokwenda itazidi kubadilika. Pia kama hujatembelea blogu ya Kona Yangu ambayo iko kwenye safu ya blogu za Wana Afrika Mashariki upande wa kuume ndani ya blogu hii, kongoli hapa uitembelee.

Iwapo kuna mtu yeyote anayetaka kuwa na blogu au ana maswali yoyote juu ya blogu (yawe ni maswali ya kitaaluma, kitaalamu, au vinginevyo) wasiliana nami nitafanya niwezalo kukusaidia. Niandikie: ughaibuni@yahoo.com au kama uko Marekani unaweza kuongea nami: 419-699-8085.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com