6/29/2004

wazungu washenzi kweli

Yaani wazungu wakisikia Afrika wanafikiri ni kama Ethiopia miaka ya 80 au Rwanda wakati wa mauaji ya halaiki. Wanadhani kila kukicha tunakatana mapanga au tunagalagala chini tukisubiri kufa kwa njaa kali. Tazama nchi kama Marekani, watu zaidi ya milioni mbili wako jela, watu zaidi ya milioni 40 hawana bima ya afya (hawa ni wale vibogoyo, kwa mfano, maana hawana hela ya kwenda kwa daktari wa meno!), idadi ya watu wasio na makazi ni kubwa kuliko nchi yoyote ya ulimwengu wa kwanza, watoto wanaoishi ghetto wanakula jumatatu hadi ijumaa chakula kingi maana jumamosi na jumapili nyumbani hakuna chakula, kwa mwaka watu zaidi ya 15,000 wanauawa kwa bunduki, watoto zaidi ya 100,000 wanatekwa...huu ni ulimwengu wa kwanza au wa kumi? Ubepari unaficha mengi. Majumba, sinema, magari, barabara nzuri vinaficha umasikini na unyama wa mfumo huu. Ni kama Afrika Kusini. Majengo mazuri, barabara za kisasa lakini Johannersburg, kwa mfano, inajulikana kama "rape capital of the world." Kila dakika anabakwa mtu! Ukiacha Moscow hakuna jiji lenye uhalifu kama Johannersburg. Lakini tazama mandhari yake.

2 Maoni Yako:

At 6/29/2004 08:29:00 AM, Anonymous Anonymous said...

Ukiishi nawo ndio utawajua

 
At 7/01/2004 06:39:00 AM, Anonymous Anonymous said...

mzungu yule wa wakati wa utumwa na ukoloni ni huyu huyu wa leo. dharau kweli!

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com