6/26/2004

Mlio wa mtutu na sauti ya muazini

Wakati nikiishi Dar, kila asubuhi na jioni nilisikia sauti ya muezzin (muazini) akiita Waislamu wakasali. Niliishi hatua chache toka msikitini (pale Tabata na Mbagala). Sauti ya "Swalaaaa....," ilikuwa ikisikika kama vile anayeomba yuko dirishani. Sasa hapa Marekani, kila jioni na asubuhi nasikia sauti ya risasi na ving'ora vya magari ya polisi na magari ya wagonjwa. Hizi risasi sijaweza kujua zinatokea wapi. Ninahisi kuna kambi karibu na hapa ninapoishi, barabara ya Uwanja wa Ndege, nje kidogo ya mji wa Toledo, Ohio. Ule mti niliosema unanitisha, kuwa unaweza kutuangukia chumbani siku moja, bado upo umesimama. Asubuhi ya leo niliutazama weee....

1 Maoni Yako:

At 6/27/2004 01:35:00 PM, Anonymous Anonymous said...

Sasa bwana Macha unafanya nini huko kwenye risasi kila siku badala ya swala??

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com