6/29/2004

IRAKI, eti ni nchi huru sasa!

Eti Iraki iko "huru" sasa. Katamka Rais, mwizi wa kura, wa hapa Marekani, Bwana Kichaka (Bush). Hii ni sawa na Afrika Kusini ambako watu weusi wanatawala kisiasa ila nguvu za kiuchumi, ambazo ndizo nguvu halisi, ziko mikononi mwa Makaburu ambao wanainunua Tanzania kwa kasi ya mwanga. Uchumi wa Iraki, ninamaanisha mafuta, uko mikononi mwa makampuni ya Amerika. Ni Wamarekani ambao watakuwa wanatoa maamuzi makuu juu ya sera na biashara ya mafuta. Hii dunia ya uongo, tufanyeje? Nyanyuka mlalanjaa!

1 Maoni Yako:

At 6/29/2004 07:42:00 AM, Anonymous Anonymous said...

Marekani ndio anajifanya bwana mkubwa wa dunia. Anachosema ndicho.

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com