8/20/2005

Sijui Niende Mashindano ya Madevu...

Mashindano ya kimataifa ya madevu yanafanyika mwezi wa kumi mwaka huu. Kama Osama na Mullah Omari (yule kiongozi wa Talibani mwenye jicho moja) wanakwenda itabidi nisiende maana najua sitaweza kuwashinda. Nitamuuliza Maalim Seif wa CUF kama ana mpango wa kwenda. Nakumbuka wakati Salimin Amour (nimesahau kumwita, Dakta) akiwa rais wa Zanzibar walikuwa wakirushiana madongo na Maalim Seif. Basi Salmin akamwambia Seif akanyoe kwanza madevu kabla ya kuanza kuota kuwa rais wa Zanziba. Maalim Seif akajibu mapigo akasema, "Kwetu wasio na ndefu makazi yao ni jikoni sio ikulu kuongoza nchi!"

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com