8/19/2005

Teknohama na mabadiliko ya jamii

Teknolojia ya habari na mawasiliano inabadili mambo kila kukicha. Kwa mfano, ile dhana mpya ya "uandishi wa umma" imepanuka. Dhana hii kwa kifupi ni kuwa kutokana na ugunduzi wa zana mpya za habari na mawasiliano, uandishi wa habari umekuwa sio tu kazi ya "waandishi wa habari" bali kila mwananchi mwenye jambo la kusema, kuhoji, kutaarifu, n.k. Sasa hata upigaji picha za kwenye magazeti sio kazi ya wapiga picha waliobobea. Mtu yeyote anaweza kuwa mwandishi wa picha na hata akatengeneza senti. Hata wewe ukitaka unaweza kutengeneza noti kama una jicho la picha. Kongoli hapa.
Mabadiliko mengine ni yale yanayotokea katika gazeti moja kule Seattle ambapo maoni ya mhariri hayaandikiwi tu na wahariri bali yanaandikwa kwa ushirikiano kati ya wahariri na wasomaji. Nenda hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com