8/13/2005

Sauti za Dunia zimekuwa za 'kidunia"

Mradi wa Sauti za Dunia (Global Voices) umekuwa wa kidunia. Ethan anatuambia kuwa mradi huu ambao una nia ya kutoa uwanja kwa wanablogu kutoa maoni na kupashana habari bila kupitia ukiritimba na vizingiti vinavyowekwa na dola na tawala za kidhalimu umekua kwa kasi toka ulipoanza miezi saba iliyopita. Kwa kipindi hiki haya yametokea:
- blogu ya mradi huu imetembelewa na watu zaidi ya 7000 kwa siku
- mwezi wa saba pekee ulikuwa na watu robo milioni waliotembelea ukurasa wa Sauti za Dunia
- blogu ya Sauti za Dunia ni kati ya blogu 200 zinazotajwa sana duniani
- blogu hii ilikuwa ni kati ya blogu 100 zilizotajwa kwa wingi kwa mwezi uliopita
- kwa mwezi uliopita wanablogu katika nchi 36 wanaoandika kwa lugha 11 wameelekeza viunganishi kwenye blogu ya mradi huu
Ethan pia anatuambia juu ya chaguo la Yahoo la mradi huu.

Soma aliyoandika Ethan katika blogu yake na pia katika blogu ya Sauti za Dunia.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com