8/04/2005

Barua Toka Kwa Mchungaji

Nimeandikiwa barua hii toka kwa mchungaji (au ni mwinjilisti?). Anajijua. Niliandikiwa nilipokuwa nimetupa mkono blogu. Isome kisha cheka:

Barua toka kwa mchungaji
Rudi kundini angalau tujue u mzima au vipi. Tutakutenga sasa na hatutakulisha chakula cha bwana mpaka utakapoanza tena kutoa sadaka ya ahadi. Nakukumbusha pia kama hutoi ahadi mtoto wako hatabarikiwa wala hatutambatiza. nakukumbusha pia kwamba mwaka jana hukutimiza ahadi yako uliahidi 20,000 ukatoa 15 ujue kuna deni la sivyo hutapata huduma za kiroho. Mwaka huu hujajaza fomu ya ahadi pia ni lazima uahidi utatupa ngapi ili tuweke kwenye mahesabu yetu. Nakukumbusha pia tarehe 34/13/28910 kutakuwa na sadaka ya mavuno safari hii ujue ni kahawa kwani miezi iliyopita kulikuwa na sadaka ya mavuno ya mahindi. Usijali sana kama huna kahawa utaweza pia kutuletea chochote hasa mahindi kwa sababu ndizi hazina bei. Pia tunakumbusha umuhimu wa kutoa noti kanisani kama sadaka kwani hizi shilingi zinakuwa nzito sana halafu zinatoboa mifuko. Tatizo jingine ni kwamba shilingi zinapoteza muda wa wazee wa kanisa kuhesabu.
Mungu wa Yakobo Isaka na Ibrahim akubariki uingiapo na utokapo sasa na hata milele hasa utakapokuwa umetimiza sadaka yako ya ahadi na mavuno.
Wako Mchungaji wa Usharika

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com