8/04/2005

Ukipewa zawadi ya kanga lazima uivae?

Msomaji Oscar Munishi kanichekesha sana. Kaniachia ujumbe hapa bloguni kufuatia niliyoandika jana kuhusu Kikwete ambaye ni muislamu kupewa biblia ili aongoze Tanzania. Mifano ya Munishi imenipendeza na nimeamua niiweke hapa kwani unaweza ukawa hujasoma maoni yake. Siweki kila alilosema naweka mifano yake miwili. Ninadhani anamaanisha kuwa Kikwete kupewa biblia inaweza kuwa ni jambo la mfano tu, hiyo biblia huenda ikakusanya vumbi bila kutumiwa. Huyu ndio Oscar Munishi:
mr ndesanjo nikikupa zawadi ya kanga leo je wewe ni lazima uivae? nikikupa panga leo kwani nimekuambia utumie kuchinja nalo watu au ukatie kuni? au ni lazima ulitumie?

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com