10/21/2005

Pop!Tech: Rebecca wa Global Voices anaongea

Rebecca ndio kamaliza na tunakwenda kula. Baadhi ya aliyosema ambayo nimeandika kwa haraka haraka ni haya:
China watu 60 wako ndani kwa kupinga serikali mtandaoni.
Tovuti ya mashirika kama Human Rights Watch huwezi kuzipata ukiwa China.

Yahoo! walishirikiana na serikali ya China kutoa taarifa za mwanaharakati wa China aliyekuwa akitumia barua pepe kueneza habari za kupinga serikali. Mwanaharakati huyu ametiwa ndani. Atasota huko kwa miaka 10.

Simu za mkono zinatumika kama watu nchi nyingine wanavyotumia kompyuta. Watu wengi China, hasa vijijini, wanatumia simu zao za mkono kusoma blogu, kuandika barua pepe, na mambo mengine ambayo unaweza kufanya ukiwa na kompyuta.

Tatizo anasema ni kuwa kampuni kubwa kama Microsoft na Yahoo! zinashirikiana na serikali ya China kutumia teknolojia za kuchunguza wananchi wa China wanafanya nini mtandaoni. Anasema tabia hii ni hatari sana maana kama makampuni yanawekeza mamilioni kujenga mitandao na teknolojia za habari na mawasiliano lakini wakati huo huo teknolojia hizo zinatumika kuzima upinzania. Uhusiano huu wa makampuni ya biashara na serikali zisizopenda upinzani unatisha.

Sasa anajibu maswali. Anasema kuwa Intaneti ilipoingia China, watu wengi walianza kusema kuwa teknolojia hii ndio italeta mwamko wa kuiangusha serikali ya kikomunisti ya China.
******
Soma aliyosema hapo awali kwa kubonyeza hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com