2/02/2005

TAZAMA HALI HALISI...

Kuna wimbo mwingine wa Bob Marley ambao unaendana sana na mambo yanayotokea leo duniani. Anasema (kipande kidogo cha huo wimbo):
Tazama hali halisi, taifa lapigana na taifa jingine
Yote haya yalianzia wapi?
Lini itaisha?
Haya, inaonekana kama uharibifu wa kila kitu
Ndio suluhisho la mambo.....

Ukiwapa inchi, watachukua yadi,
Ukiwapa yadi, watachukua maili...
Sasa hakuna atakayeweza kuwazuia...

Hizo ndio hisia za Bob. Pale anaposema kuwa hawaridhiki, wanataka zaidi (ukiwapa yadi wanataka maili) anakuwa kama anawazungumzia jamaa zetu wanaotaka kutawala dunia nzima na kuweka mirija ya kunyonya mafuta kila kona!

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com