2/02/2005

SHARON STONE ANAONEA HURUMA WATANZANIA??

Mpe mcheza filamu Sharon Stone dakika kumi uone atafanya nini! Kwa dakika tano alitengeneza dola milioni moja kwa ajili ya malaria nchini Tanzania. Inaelezwa kuwa wakati maafa ya "tsunami" ya malaria yakielezwa katika mjadala ambao Rais Benjamin Mkapa alikuwa mmoja wa wazungumzaji, ghafla Sharon Stone alisimama na kumwambia Mkapa kuwa anatoa dola 10,000 kusaidia Tanzania na kuwataka wengine ukumbini wafanye hivyo.

Kati ya sinema ambazo Sharon Stone ameshiriki ni Stardust Memories (1980), Police Academy 4: Citizens on Patrol (1987), King Solomon's Mines (1985), Irreconcilable Differences (1984), Basic Instinct (1992), The Muse (1999), Diabolique (1996), If These Walls Could Talk 2 (2000), n.k.
Habari nzima hii hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com