11/26/2004

BABA MOI, BABA MOI, BABA MOI!!!

Mahakama Kuu nchini Kenya imeamua kuwa "Baba" Moi na wenzie (akiwemo mwanaye Philip) lazima watoe ushahidi katika uchunguzi wa kashfa ya Goldenberg. Hukumu hii inafuatia kesi iliyofunguliwa na wanaharakati waliodai kuwa uchunguzi huo lazima usikilize ushahidi toka kwa watu hawa. Mambo kama haya yanapotokea Afrika yananifanya niwe na furaha mwezi mzima. Hii tabia ya kuona kuwa mtu akiwa ameshika cheo cha juu serikalini hatakiwi kuhojiwa, kufikishwa mahakamani au mbele ya tume za uchunguzi inachochea rushwa, wizi, uzembe, na ulaghai. Ni tabia mbovu kabisa isiyohitajika barani kwetu. Tanzania nako lazima tubadili sheria inayozuia, kwa mfano, Rais kufikishwa mahakamani. Ukimpeleka Rais mahakamani unaambiwa, "Huwezi kumshtaki Rais wakati akiwa madarakani." Ukisubiri hadi atoke madarakani kisha ukampeleka mahakamani utaambia, "Sheria inasema kuwa huwezi kumshtaki Rais kwa makosa aliyofanya wakati akiwa madarakani." Jamani!
Mtu mwenye wadhifa kama Rais akiwa haogopi nguvu ya sheria (na jela), ni vipi tutanajenga uaminifu na uwajibikaji? Hakuna haki ya raia yeyote Afrika anayepaswa kuwa juu ya sheria (sio Rais wala Rais mstaafu).
Soma habari hiyo hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com