10/06/2004

UKIMWI NA AFRIKA

Afrika na ukimwi ni kama pacha katika fikra za watu wengi huku ughaibuni. Wanashindwa hata kuona wenzao wanaotokomea kwa gonjwa hili kwa kudhani kuwa ugonjwa huu (ambao wanadai umetoka afrika) unawamaliza Waafrika peke yao. Sasa jana kulikuwa na kiti moto cha wagombea umakamu wa Rais, Dick Cheney na John Edwards. Wakaulizwa juu ya athari za ukimwi miongoni mwa wanawake weusi. Muulizaji akasema wazi kuwa hataki wazungumzie Afrika, bali Marekani. Wapi! Jamaa hawa wote wawili wakaanza kuelezea jinsi ambavyo ugonjwa huu ulivyo na madhara katika mataifa ya Afrika na kwingineko katika uliwengu wanaouita wa tatu. Dick Cheney alipobanwa juu ya Ukimwi miongoni mwa wanawake weusi ambao ni rahisi kuupata ukilinganisha na wanawake wengine Marekani, alisema, "Sina taarifa hizi kuwa ukimwi ni tatizo kubwa kwa watu weusi hapa Marekani!" Yaani makamu wa rais mzima anajua zaidi tatizo la ukimwi na takwimu zake Afrika kuliko hapa Marekani.

Dick Cheney alibanwa na John Edwards pale alipoambiwa kuwa rekodi zinaonyesha kuwa alipiga kura ya kuzuia kufunguliwa kwa Nelson Mandela na pia kupinga kuwepo kwa sherehe ya kitaifa ya Martin Luther King. Maaluni mkubwa huyu....alikuwa akiunga mkono ubaguzi wa rangi Afrika Kusini sasa anajifanya eti anapenda haki za binadamu ndio maana anatuma majeshi huko Iraki yakawakomboe Wairaki.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com