10/02/2004

TUMERUHUSIWA NA NYERERE KUVUTA BANGI!!

Ingawa nimebanwa na shughuli kutokana na muda mfupi nilionao kabla ya kurudi Toledo, Ohio, habari hii nimeisoma muda mfupi uliopita nimeona niiweke hapa ili wale ambao hawajaisoma waisome. Imeniacha hoi kabisa. Bonyeza hapa ili upate uhondo wenyewe.
Nimekutana na mmasai mmoja, Kakuta Ole Hamisi, nilipotembelea soko la "kiboriloni" la Vermont. Hili ni soko la kila jumamosi. Lilianza mwaka 1974. Nilikuwa hapo na bwana Kakuta ambaye anapenda kuita wazungu, "mabeberu." Kama nilivyoahidi, katika makala yangu ya wiki hii gazeti la Mwananchi, nitazungumzia safari hii. Kwahiyo nitagusia habari za Kakuta na hili soko. Haya, bonyeza hapo juu usome kisa cha kabila la Wahadzabe ambao ukiwatembelea ni vyema ukakumbuka kuwapelekea zawadi ya bangi!

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com