6/16/2004

Vitabu vya Nyerere

Siku hizi naulizwa maswali makali makali juu ya Tanzania. Nimeulizwa, "Hivi vitabu alivyoandika Mwalimu Nyerere vinatumiwa shuleni?" Jibu ni kuwa sijui. Sidhani. Kwa jinsi ninavyojua nchi yangu, sidhani. Utasikia watu wakisema Nyerere Baba wa Taifa lakini ukiwauliza maana yake ni nini hasa midomo inacheza. Watanzania kama taifa bado tunacheza. Sijui ni jambo gani ambalo tunalifanya kwa uhakika na makini. Watu wa maneno meeeeeengi. Tunapenda maneno sana. Tunakwenda kwenye mikutano ya siasa. Wanasiasa wanatuuzia maneno. Tunashangilia kweli na kuwachezea ngoma na kuimba huku tukiungua jua. Wao wako kivulini. Waongo wote. Sio wa upinzani. Sio watawala. Waongo watupu.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com