10/22/2005

Pop!Tech: Falsafa na mengineyo

Watu wametoka kwenye pumziko. Sasa tunapata dozi ya falsafa toka kwa mwanafalsafa na mwanahesabu, Nassim Taleb. Sijui kama nitaweza kusikiliza vyema. Kuna mengi yanaendelea. Ninatazama teknolojia ya kufundishia mtandaoni toka kwa mwalimu mmoja hapa pembeni yangu. Bonyeza hapa uone shirika analofanya kazi. Anaandaa kompyuta yake ili aniingize kwenye darasa lake (liliko mtandaoni). Nimekuwa namuona kila dakika yuko bize akiandika. Nikamuuliza, mbona? Nilidhani ni mwanablogu kumbe mwenzangu tuko wote hapa lakini wakati huo huo anafundisha wanafunzi waliotapakaa sehemu mbalimbali duniani! Mwanablogu wa Kenya, Ory (Kenyan Pundit) yuko mbele yangu upande wa kulia akihojiwa na Renee Blodget (ambaye ameishi Tanzania na hata kulala lupango!). Anamuhoji Ory kwa ajili ya blogu yake hii hapa. . Kesho asubuhi Waafrika wote 12 tulioko hapa tutakuwa kwenye kiti moto kwa ajili ya kipindi cha luninga kituo cha PBS. Tulikuwa na mkutano kabla ya chakula cha mchana kujadili jinsi ambavyo kiti moto kitakavyoendeshwa. Mwendeshaji wa kiti moto atakuwa ni David Kirkpatrick ambaye ni mhariri wa masuala ya intaneti wa jarida la Fortune. David ni kati ya wazungu wachache ambao wameweza kutamla jina langu inavyopaswa bila kuketishwa chini na kufundishwa kwa kiboko. Labda ni kwakuwa aliwahi kuishi Afrika (Nigeria) na ametembelea nchi mbalimbali za Afrika ikiwemo Tanzania.
Huyu mwanafalsafa naona anawaacha wengi nje...wanaoanza kusinzia ni wengi. Wapiga miayo nao wamo...wanafalsafa wakati mwingine...anakuwa kama anaongea mwenyewe.
Baadaye.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com