10/22/2005

abPop!Tech: Sam Harris na Tatizo la Dini

Anaongea Sam Harris:
- dunia imejaa imani ambazo hazikubaliani
- dini kuu zimetokana na vitabu vilivyoandikwa na watu
- nitaongea mambo kadhaa ambayo yanaweza kukera baadhi ya watu
- najua kuwa watu asilimia 90 wanamwamini mungu, asilimia 93 wanaamini kuwa Yesu alifufuka, kwahiyo lazima nitaudhi baadhi ya watu maana nitaongea mambo makali sana dhidi ya dini na imani
- asilimia 22 ya Wamarekani wanaamini kuwa Yesu atashuka toka mawinguni na kuokoa dunia hii hivi karibuni
- Wamarekani wanaamini kuwa Israeli ni nchi iliyotengwa na mungu kwa ajili ya waisraeli
- asilimia zaidi ya asilimia 50 wanaamini kuwa binadamu wanaamini kuwa ni kweli kabisa kuwa tuliumbwa toka kwenye udongo, wanaamini kisa cha nyoka kuongea na kumshawishi Hawa kula tunda
- chukua mfano huu: eti matumizi ya kondomu ni kinyume na mapenzi ya mungu. Nenda Afrika katika vijiji ambavyo mamilioni wanakufa, nenda huko ukasambaze imani hii. Huu ni ujinga na kosa la jinai
- ninachosema ni kuwa lazima fikra na imani potofu zipewe changamoto. Sitaki kukataza watu kuwa na imani hizo au kupitisha sheria dhidi ya imani hizi. Ninachotaka ni watu kuhoji imani na fikra hizo
- tatizo la dini ni kuwa dini hazitaki hoja au ushahidi
- ndio unaona tofauti ya sayansi na dini, kwenye sayansi lazima kuwe na ushahidi. Unaona wakristo wenye siasa kali Marekani wanasema kuwa shambulio la Septemba 11 linatokana na ghadhabu ya mungu kutokana na Marekani kuwa na mashoga na kuruhusu utoaji mimba
- hivi wako wapi magaidi wa kujitoa mhanga wa Kibudha? Unatakiwa kufanya kazi kubwa sana kupata watu wa kujitoa mhanga katika imani ya Kibudha
- nashindwa kuelewa kwanini watu wenye siasa za kushoto hawataki kukubali kuwa uislamu una itikadi inayofanya rahisi kwa waumini wake kujitoa mhanga na kuua wasio na hatia
- kwenye uislamu kuna imani kuwa wanaojitoa mhanga wanapata maisha ya raha ya milele
- vitabu vya dini havifundishi uvumilivu wa dini na imani tofauti na yako. Vinafundisha ukereketwa na siasa kali. Hakuna kitabu cha dini kinachosema dini zote zina haki sawa
- wakristo waliokuwa wakichoma watu moto
- "Mtakatifu" Aquinas alisema kuwa wanaopinga ukristo hawana budi kuuawa. "Mtakatifu" Augustine alisema kuwa wateswe vikali sana
Maswali:
Anaulizwa anafikiria nini kuhusu "intuition"
- anajibu na kusema kuwa tunazungumzia "intuition" pale tunaposhindwa kuelezea hisia fulani
Anaulizwa swali kuhusu maendeleo ya binadamu na imani ya dini
- anajibu kwa kusema kuwa ukitazama ripoti ya Umoja ya Mataifa ya Maendeleo inayotolewa kila mwaka inaonyesha kuwa nchi ambazo zina maisha bora zaidi (kwa vipimo kama afya, elimu, vitendo vya uhalifu, vifo vya watoto, usawa wa jinsi, n.k) ni zile ambazo zina watu wengi wasio waumini wa dini (Mawazo yangu: huenda huyu bwana kasoma makala zangu maana hii ni hoja yangu!)
Mwisho***

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com