10/22/2005

Pop!Tech: Jamaa wa Architecture for Humanity

Anaongea Cameron Sinclair. Huyu ni mwanzilishi wa shirika la Architecture for Humanity.
Shirika lake lina miradi sehemu mbalimbali duniani. Shirika hili linabuni na kujenga makazi katika maeneo yenye maafa, kwa mfano, wamejenga zahanati zinazomfuata mgonjwa kwa ajili ya wagonjwa wa Ukimwi Kusini mwa Afrika, makazi ya wakimbizi wanaorudi makwao, majengo ya michezo.

Haya ndio anayosema:
- wanajenga uwanja wa mpira wa miguu kwa wanawake nchini Afrika Kusini
- ramani ya uwanja hiyo ilibuniwa na vijana walioshiriki kwenye mashindano ya kuchora ramani ya uwanja huo. Aliyeshinda ni kijana toka Singapore mwenye miaka 20
- sababu kubwa ya kujenga uwanja huo ni kuwa wanawake katika kitongoji cha Somkhele, KwaZulu Natal hawana maeno ya kupumzika na kujishusisha na michezo. Pia idadi ya walioathirika kwa ukimi ni kubwa sana. Ili kuepusha vitendo ambavyo vinaweza kuwaweka kwenye hatari ya kupata ukimwi, wakazi wa kitongoji hicho waliamua kuwa eneo la michezo kwa wanawake ni muhimu
** Anatuonyesha picha na video za miradi yao katika nchi mbalimbali duniani
Anaonyesha picha ya nyumba ambayo inaweza kuangushwa na kisha kujengwa kwa dakika 45! Nyumba hii haiwezi kuteketea kwa moto. Anaonyesha picha nyingine ya shule iliyojengwa kwa fedha zilizotokana na mandazi yaliyouzwa na watoto wa shule. Shule hi imejengwa kwa teknolojia ambayo inakusanya maji ya mvua kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

*** Anaonyesha video: inaanza na kauli toka kwa mtu anayesema kuwa Bush hapendi watu weusi. Video ina wimbo wa rap na picha za maafa ya Katrina. Wimbo huu wa rap ni kuhusu maafa ya Katrina. Sijawahi kuusikia. Una maneno makali sana.

** Anaonyesha picha ya nyumba za bei nafuu ambazo wamezibuni kwa ajili ya wakazi wa New Orleans.

(Bwana anaongea haraka kweli!)
- anasema kuwa mtu mmoja katika saba duniani anaishi kwenye makazi yasiyofaa kabisa kuishi kwa mwanadamu.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com