10/21/2005

Pop!Tech: Negroponte na kompyuta za dola 100

Nitakuwa naandika haraka anayosema Nicholas Negroponte:
- ukitaka kubadili maisha ya watu badili mfumo wao wa elimu
- nia yake ni kujenga kompyuta ya mapajani ya dola 100
- asilimia 50 ya bei ya kompyuta za mapajani inakwenda kwenye mambo ambayo hayahusiani na utengenezaji wa kompyuta hizo.
- mwanzoni walitaka badala kuweka kioo kwenye kompyuta hizo ili kupunguza gharama watumie aina ya karatasi ngumu!
- kompyuta hizo zitakuwa pia ni kitabu
- wamekwenda nchi hizi kutangaza mradi wao: China, Brazil, India, Thailand na wanaongea na Afrika Kusini na Nigeria
- watu wengi wanamwambia kuwa yeye ni mwalimu wa chuo kikuu hajui masuala ya uzalishaji wa bidhaa. Anadai kuwa amekuwa kwenye bodi ya kampuni ya Motorola kwa muda mrefu kwahiyo anafahamu kwa kiasi fulani masuala ya uzalishaji wa bidhaa
- Anaweza kuwa wanaweza kushinda kutimiza ndoto yao ila kushindwa kwao hakutamaanisha kuwa kompyuta hizo hazitatengenezwa bali labda watazitengeneza kwa dola 125, kitu kama hicho ila sio kutozitengeneza
- wanaanza kuzitengeneza mwezi wa pili mwakani
(anatuonyesha picha za kompyuta hizo zitakavyokuwa)
- Kompyuta hizo zitakuwa zikitumika kama tunavyotumia kompyuta hivi sasa na pia kama kitabu. Yaani kama unavyoshika kitabu mkononi kukisoma, utaweza kuishika kompyuta hiyo kama kitabu
- wataonyesha kompyuta hizo mwezi ujao kule Tunisia kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Jamii-Habari
** Amemaliza. Maswali baadaye.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com