6/26/2005

Mdahalo kuhusu Afrika na G8 redio ya BBC

Siku ya ijumaa na jumamosi, tarehe kwanza na pili mwezi ujao, Redio ya BBC itatangaza mdahalo uitwao: Je nchi za G8 zinaweza kuinusuru Afrika? Watakaoshirika katika mdahalo huo utakaofanyika katika ukumbi wa Africa Centre, jijini London, ni: Tajudeen Abdul-Raheem, Mkurugenzi wa Justice Africa na katibu mkuu wa Pan African Movement, Rosemary Museminali,balozi wa Rwanda Uingereza, James Shikwati, mwanauchumi toka Kenya, na Lord David Triesman, waziri mtarajiwa wa masuala ya Afrika.

Matangazo ya mdahalo huo yatarushwa siku ya ijumaa tarehe kwanza saa 1900 GMT, 2100 GMT, na 2200 GMT; na siku ya jumamosi tarehe pili saa 1100 GMT.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com