6/19/2005

UCHAGUZI WA IRANI, MGOMBEA MWENYE BLOGU NA KADHALIKA

Mwanablogu maarufu wa Iran anayeishi nchini Kanada, Hoder, yuko nchini Iran ambako alirudi hivi karibuni ili aweze kuandika juu ya uchaguzi huo. Pia mmoja wa wagombea urais nchini humo, Dakta Mostafa Moeen, ana blogu yake. Kulikuwa na hofu kuwa pengine mwanablogu Hoder angetiwa ndani kama wanablogu wengine ambao wako jela kutokana na kutumia blogu zao kupinga udhalimu wa serikali yao.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com