6/13/2005

MADENI...WALIKOPA LINI?

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, kati ya mwaka 1970 hadi 2002, Afrika ilipokea mikopo yenye thamani ya dola za Kimarekani bilioni 540. Katika kipindi hicho, Afrika ililipa wazungu waliotukopesha dola bilioni za Kimarekani 550. Hadi mwaka 2002, Afrika ilikuwa na madeni ya dola za Kimarekani 295.
Nadhani mmeona vichwa vya habari kuhusu nchi 14 za Afrika zilizosamahewa madeni asilimia 100, Tanzania ikiwa ni mojawapo. Tanzania ilikuwa ikitumia asilimia 12 ya pato lake kulipia madeni. Watawala wa nchi zilizosamehewa madeni wanadai kuwa serikali zao sasa zitaweza kutumia fedha hizo kwa maendeleo ya wananchi.
Mimi hadi hivi sasa kuna jambo moja sijaelewa. Kwanini tunasamehewa madeni? Kwani tulikopeshwa lini? Mbona hizo hela mimi sijaziona? Kama fedha tulizokopa ziliingia kwenye mifuko ya watawala wanaotupa takrima kisha tunawapa kura, fedha zitakazopatikana kutokana na msamaha huu ndio wataamua kuzipeleka kwa Hadija, Matayo, Buruani, na Msechu?
Kusamehewa madeni huku wezi wakiwa wamekalia viti vya uongozi kutasaidia nini? Swali hilo.

2 Maoni Yako:

At 6/14/2005 03:36:00 AM, Anonymous Anonymous said...

Hili ni swali muhimu zaidi: 'walikopa deni lini? Tena walifanya nini na hela hizi?

 
At 6/14/2005 01:14:00 PM, Anonymous Anonymous said...

swali la msingi ndio hilo, madeni hayo yalifanyia nini?

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com