4/08/2005

SAMAHANINI KUHUSU MAKALA ZA PADRI NA FREDDY

Ninawaomba samahani wale wote walioniandikia wakiuliza juu ya kuchelewa kuweka makala za Padri Karugendo na zile za Freddy Macha nilizowaahidi. Nina makala zao nyingi na zenye ujumbe mzito kwetu sote. Nitapandisha moja moja kadri muda unavyoruhusu. Pia nitajibu barua pepe zenu zote, ingawa nitachelewa. Ombi la kuweka baraza la majadiliano nimelipokea. Ngoja nitumie lugha ya "wana si-hasa": ombi lenu linashughulikiwa.
Mada ninayoandaa imenikamata hasa. Nina rundo la machapisho ya kusoma, vitabu, tovuti za kutembelea, na wanablogu wa kuwasiliana nao. Mniwie radhi nikitokomea. Tuko pamoja. Tuendelee kunoa akili zetu na kusafisha ukurutu wa kasumba, utegemezi, na kutokujiamini. Wakati ni huu.
Kuna barua kadhaa za wasomaji na marafiki zangu ambazo nimezipenda mno. Nazo nitazipandisha hapa mzisome. Zitakuwa chakula murua kwa ajili ya fikra zetu.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com