4/10/2005

MAKALA NA HADITHI TOKA KWA FREDDY MACHA

Nimeweka makala mpya na hadithi toka Uingereza kwa Freddy Macha. Kuna hadithi aliyoiandika mwaka 1976 pale Buguruni, jijini Dasalama iitwayo Balaa! Bonyeza hapa uisome. Pia kuna makala aliyoandika kuhusu mwanamuziki mahiri wa Tanzania King Kiki wakati alipotembelea Uingereza. Isome hapa. Kingi Kiki ndiye aliyeimba, "Mimi msafiri bado nipo njia, sijui lini nitafika. Ninaulizia kule ninakokwenda..." Halafu kuna makala (sehemu ya kwanza hadi ya tatu) kuhusu umuhimu wa wanawake kujifunza sanaa ya kujilinda (martial arts). Zisome hapa, hapa, na hapa. Usisahau kuwa makala zake nyingine ziko katika kona yake hapa ndani blogu. Zitazame upande wa kuume wa blogu hii chini ya makala zangu.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com