4/13/2005

BLOGU NYINGINE YA KISWAHILI HIYOOO!

Kuna mwanablogu mpya wa Kiswahili, Egidio Ndabagoye, toka Moshi, Tanzania. Katika blogu yake anasema: Wanaozungumza hawajui, wanaojua hawazungumzi! Pia anatukumbusha kuwa Edward Moringe Sokoine alifariki tarehe 12 mwezi wa nne. Anauliza kama kuna anayemkumbuka. Blogu za Kiswahili zinaongezeka polepole. Moja baada ya nyingine. Polepole ndio mwendo. Mwenda pole hajikwai, akijikwaa haanguki, akianguka haumii. Haraka haraka haina baraka. Kidogo kidogo hujaza kibaba...mababu walitufunza. Mtembelee mwanablogu huyu hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com