1/24/2005

SUMAYE NA ULAJI

Mimi nadhani kuwa watu wanatania tu. Kwani Sumaye mwenyewe amewahi kusema kuwa anataka ulaji namba moja? (ulaji namba moja ni urais.) Nimekuwa nikisikia akitajwa kila mara kuwa ni kati ya watu watakaogombea nafasi ya kuwa mgombea urais, yaani ulaji, katika chama twawala. Mimi nabisha kabisa. Najua Sumaye ana busara kiasi fulani. Yaani mnataka kuniambia kuwa Sumaye hafahamu kuwa urais wa nchi yenye mzigo wa matatizo, shida, na tabu kama Tanzania hatauweza? Hebu acheni hiyo.
Kwani Sumaye katika uwaziri mkuu wake amefanya mambo yapi hasa ambayo yamegusa nyoyo za Watanzania kiasi ambacho waamke asubuhi na mapema kwenda kumpigia "kula"? Najua kuna mambo mawili makubwa ameyafanya katika kipindi chake cha uongozi:
1. Ameweza kuitetea sirikali bungeni dhidi ya wale wote wanaoipinga na kuisakama.
2. Amekuwa kila mara katika hotuba zake akitukumbusha kuwa, "Sirikali yenu inafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha mnakuwa na maisha bora" huku taa za ofisini kwao na majumbani zikiwa zimezimwa usiku. Hizo kazi wanazofanya usiku wanazifanyaje gizani?Au labda wanafanya kwa uweza wa kimiujiza. Au kuna kazi "fulani" wanazofanya "kwa ajili yetu" ambazo huwa hazihitaji taa!
Sumaye, hiyo sirikali "isiyolala" ni ya Tanzania ninayoijua mimi (iliyopakana na Kenya na Uganda) au ni nyingine?
Hii habari hapa ndio imenifanya kuandika haya yote.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com