12/14/2004

UNAWEZA KUNISAIDIA?

Tafadhali sana nisaidie. Nashindwa kuelewa. Ziwa "Victoria" linafanya nini Tanzania? NInakubali kuwa nchi yetu ni masikini (ingawa kwa ni tajiri sana kimali asili), lakini umasikini wetu kiuchumi unatuzuiaje kuenzi watu wetu kwa kutumia majina ya mashujaa, manabii, wafalme, machifu, malkia, waliojazana katika historia ya nchi na bara letu? Ninaposema tujikomboe unadhani ninatania? Kulipa ziwa jina linaloendeleza heshima, utu, na utamaduni wetu tumeshindwa. Kama tumekosa majina ya maana usukumani na uhayani ikabidi twende hadi Uingereza.... mbona kuna kazi? Mko yatari tusaidiane kazi hii ya kurudisha historia, utamaduni, uhai na nafsi zetu zilizotekwa? Aliye tayari anyooshe kidole...kisha aje hapa bloguni tuhangaike naye.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com