12/12/2004

ITEMBELEE SERIKALI NA BUNGE LAKO

Hii ndio tovuti ya siri-kali yako: http://www.tanzania.go.tz/index2k.html
Na hili hapa ni bunge lako: http://www.parliament.go.tz/bunge/bunge.asp

Hakikisha una kamusi mkononi ndipo utembelee tovuti ya bunge. Wabunge wetu "tumewachagua" ili watuwakilishe sisi akina Magoti, Msechu, Kulusumu, Riziwani, Msembechu, Elibariki, n.k. lakini lugha wanayotumia ni ya akina Jones, McMurray, Phillips, na Howard. Hili ndio bunge letu. Linatuuza waziwazi, mchana wa jua la saa sita. Ukikutana na Pius Msekwa naomba unisaidia kumuuliza, tovuti ya bunge la Watanzania si inapaswa kuwa katika lugha inayotumiwa na Watanzania wote? Au tovuti hii imeundwa kwa ajili ya "watawala wapya" wanaotawala kwa kidhibiti-mbali:

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com