11/16/2004

MAJANGILI YA HISTORIA NA URITHI WA WAAFRIKA

Kwa wale wanaofuatilia historia ya wizi wa urithi na mali za Waafrika uliofanywa na majangili, masinzia, na vibaka wa kimataifa wakati wa ukoloni Barani Afrika, kuna habari ya kusisimua. Italia imeamua kurejesha mnara waliouiba zaidi ya miaka 70 iliyopita huko Abisinia/Ethiopia. Bonyeza hapa kwa habari kamili.
Majangili haya yaliyokuwa yamebeba Biblia mkono mmoja huku mkono mwingine ukidokoa na kukandamiza yamekuwa kwa miaka mingi yakikataa kurudisha mali za wizi zilizoibwa wakati "wakitufundisha ustaarabu"!! Washenzi kweli, yaani wanatufundisha ustaarabu kwa huku wakituibia? Nchi ya Ethiopia/Abisinia ambayo ina historia ndefu ya kale na nzito duniani imekuwa ikipiga kampeni kubwa kwa duniani ili urithi wao urejeshwe. Chama kiitwacho The Association for the Return of the Magdala Ethiopian Treasures (AFROMET)kimekuwa mstari wa mbele katika kampeni hii. Kongoli hapa uende kwenye tovuti yao.
Kwa habari zaidi juu ya wizi wa urithi wetu uliofanywa na mabeberu wa Kibabiloni kongoli hapa na hapa na hapa na hapa na hapa na hapa na hapa . Hivi Tanzania Mijerumani na Miingereza ilituibia nini? Lini tutaanza kudai? Wana historia, akina Rehema Nchimbi, tupeni ukweli juu ya hili. Nasikia hata kichwa cha Mkwawa walichorudisha sicho. Kweli??

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com