11/13/2004

DAUDI NA GOLIATHI

Tatizo kubwa la Marekani katika ubeberu wake wa kivita huko Iraki ni kuwa, jeshi la Marekani linajua vita vya jeshi kwa jeshi. Mbinu wanazotumia, silaha walizonazo, mafunzo yao na saikolojia yao kwa ujumla ni kwa ajili ya vita ambavyo adui ni jeshi jingine ambalo wanajua liko wapi, lina silaha gani , n.k. Vita vya mtaani vinavyoendeshwa na watetezi wa Iraki ni tofauti kabisa na vita wanayoweza Wamarekani. Kutokana na sababu hii ndio maana unaona kuwa hakuna siku eti Marekani itaweza kutamka, "Tumeshinda vita." Sasa juzi wamevamia Fallujah kwa mara ya pili. Wanadai eti wameteka mji. Kumbe wakati wakiingia Fallujah, wenzao hao wakatokomea. Sasa wameingia Mosul ambako polisi wamekimbia na kuacha vituo vya polisi. Mkuu wa polisi kafukuzwa kazi baada ya vijana wake kukimbia! Wameongeza pia mashambulizi Baghdad ambapo Wizara ya Elimu imeshambuliwa. Kawaida vita vya namna hii vinakwenda kama Paka na Panya. Wamarekani wakitokea jamaa wanaingia mitini, kisha wanajitokeza baadaye. Hawa jamaa wanajua kuwa sio rahisi kupambana na Marekani ana kwa ana. Kwahiyo wanachofanya ni kuyeyuka na kuibuka. Kuyeyuka na kuibuka. Sasa baadhi ya vikosi vya Marekani vinakwenda Mosul. Wakifika huko jamaa wanayeyuka, wanakwenda pengine. Wanawakimbiza Wamarekani huko na kule. Bonyeza hapa usome habari hiyo. Kwa ufupi tunayoona Iraki ni kama hadithi ya Daudi na Goliathi. Kwa kombeo Marekani atakumbuka yaliyomkuta Vietnam na Somalia.


0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com