11/13/2004

KWA WAKUBWA TU...

Kisa hiki kiko kwenye mkusanyiko uitwao MAMBO YA NYAKATI ambao unaweza kuupata kwa kubonyeza hapa. Soma kisa hiki kama una umri zaidi ya miaka 18!!!!!!!


MSWAHILI APATA WAZUNGU

Wa kwanza alikutana naye kilabu cha usiku. Akamuuliza, “Umewahi kujaribu mtu mweusi?” Akasema hajawahi. Wakajaribu. Akapenda. Wakajaribu tena na tena na tena hadi alipohamia Columbus akamwacha New York.

Wa pili walikuwa naye darasa moja. Akamuuliza kama amewahi kujaribu watu weusi. Akasema amewahi. Akamuuliza, “Umewahi weusi wa hapa Marekani au weusi toka Afrika ?” Akasema amejaribu weusi wa Marekani. “Basi hujajaribu weusi mpaka ujaribu Mwafrika.”

Huyu naye Wakajaribu. Hadi leo wanaendelea mara moja moja.

Wa tatu walikuwa wanafanya ofisi moja. Walipenda sana kutaniana. Siku moja binti huyo akaja na kipande cha gazeti chenye habari isemayo kuwa weusi wa Afrika wana nanihii kubwa kupita watu wengine duniani. Wazungu ndio wa mwisho. Yao kiduchu kama kidole cha mtoto mchanga. “Ni kweli?” Binti akamuuliza.
“Sijui. Jaribu utajua.”
“Jumatano tusije kazini. Tafuta sababu.” Binti akamwambia.
Wakakubaliana. Ilikuwa ni jumatatu.

Alhamisi alipoamka asubuhi alijua kengele ya mlango ikilia lazima atakuwa mwenye nyumba akilalamika juu ya kelele za mwanamke usiku mzima. Laiti Kibo angejua. Kumbe usiku mzima mwenye nyumba aliweka sikio ukutani akisikiliza kwa furaha isiyo na kifani.

Wa tano alimfanya aamini kuwa weupe zimewaruka. Kabla hajahamia hapa alikuwa anakaa mtaa wa pili, gorofani. Siku moja wakati anashuka chini kuchukua nguo toka chumba cha kusafishia nguo akakutana naye katikati ya ngazi. Akawa anampita, lakini binti akasimama. “Nakuona kila siku unakaa namba ngapi?”
“Niko namba 8.”
“Unaishi mwenyewe?”
“Ndio.” Akamjibu huku akijiuliza kwanini anaulizwa hayo maswali.
“Nakuona kila siku. Huwa nakutazama lakini wewe huna habari.”
Jamaa akatabasamu. Binti akaangusha bomu la silaha za maangamizi ya hisia na uroda.
“Kama hujali twende kwako tukafanye.”

Ndio maana toka siku hiyo Kibo huwa anawaambia marafiki zake, “Wazungu hawana tofauti na wanyama wakati mwingine. Lakini uzuri wako ni kuwa hakuna kiswahili kirefu...mara kimetoka huku kikaishia kule...hiyo hawana.”

Baaadaye akaamua kurudi “nyumbani.” Akaenda kwa Sofia ambaye kahamia hapa Columbus toka Atlanta. Sofia, mtoto wa Kinyakyusa , akaja juu. “ Wewe na hao wazungu wako siku zote hutuoni. Leo imekuwaje? Wamekutema?”
“Unajua dada zetu ninyi hamna mfano.”
“Hebu acha hizo. Kwanza sote tunatafuta dokumenti, huko si kupotezeana muda bure?”

Sofia akakataa katukatu. Hana muda na Wabongo.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com