8/18/2004

NINASAFIRI

Ninasafiri leo alfajiri au kesho usiku kuelekea jimbo la Vermont. Nitarudi jumapili. Sina uhakika kama nitakuwa hewani. Ninajaribu kutengeneza blogu hii ili niweze kutuma taarifa kwa simu nawe uweze kunisikiliza kama una spika kwenye tarakilishi (computer) yako. Nimejaribu kwa lisaa limoja sasa lakini bado sijafanikiwa. Ila ninakuachia zawadi ya makala tatu mpya. Ni mpya katika blogu ila ziliandikwa muda kidogo kwa ajili ya safu yangu ya kila jumapili katika gazeti la Mwananchi. Kwa mfano, makala ya Krisimasi bila Yesu niliandika Krisimasi ya mwaka jana. Makala hizo ziko chini ya picha yangu mkono wa kuume. Nenda soma, furahia. Hadithi ya mtoto wa kichagaa na mtoto wa kizungu itaendelea.

Pia niko mbioni kuweka kamera tovuti (webcam) ili ukija kwenye blogu yangu kama niko mtandaoni utaweza kuniona. Au sio? Kwaheri. Uhuru!

2 Maoni Yako:

At 8/19/2004 10:16:00 AM, Anonymous Anonymous said...

Safari njema.

 
At 8/19/2004 10:17:00 AM, Anonymous Anonymous said...

Tutakusubiri. Hadithi malizia. Kuna kisa kingine cha hotelini hukumalizia.

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com